Bodi ya Kahawa Tanzania (TCB) ni chombo cha serikali kilichoanzishwa chini ya Kifungu cha 3 cha Sheria ya Tasnia ya Kahawa, Sura ya 347 (Toleo lililorekebishwa la mwaka 2023). Kwa mujibu wa Kifungu cha 5 cha Sheria hiyo, Bodi imepewa jukumu la kusimamia na kudhibiti sekta ya kahawa pamoja na kuishauri Serikali kuhusu masuala yote yanayohusu maendeleo ya sekta hiyo nchini.
Katika kutekeleza majukumu yake, TCB ni chombo kikuu cha udhibiti kinachohakikisha kuwa wadau wote katika mnyororo wa thamani wa kahawa wanazingatia Sheria ya Tasnia ya Kahawa, kanuni zake pamoja na viwango vinavyotumika kitaifa, kikanda na kimataifa. Aidha, Bodi inakuza uwazi, ufanisi, uhakika wa ubora na ushindani katika sekta ya kahawa, huku ikiendeleza maendeleo endelevu ya mnyororo wa thamani na kupanua fursa za masoko ya kahawa ya Tanzania ndani na nje ya nchi.
TCB inaendelea kujenga sekta ya kahawa iliyo shindani, jumuishi na endelevu, inayochangia ukuaji wa uchumi wa taifa na kuboresha maisha ya wakulima wa kahawa.

